.

.

.

.

Monday

Sudan:Mwanamke mkristo bado yu taabani

Mawakili wa mwanamke mkristo nchini Sudan ,Meriam Ibrahim wamesema kuwa watawasilisha ombi mahakamani la kutaka mashtaka ya kughushi stakhabadhi bandia dhidi ya mteja wao kuondolewa.

Bi Ibrahim alikamatwa siku ya jumanne,siku ambayo mahakama ya rufaa ilibadilisha hukumu yake ya kifo hadi kuwa ya uasi.

Kufuatia uamuzi huo alijaribu kutoroka nchini humo kupitia stakhadhi za Sudan Kusini lakini akakamatwa katika uwanja wa ndege wa Khartoum.

Wakili mmoja amekiambia kitengo cha habari cha Ufaransa kwamba ana matumaini mamlaka itamuondolea mashtaka hayo na kumpatia paspoti ya Sudan ili kumruhusu kuelekea nchini Marekani.

No comments:

Post a Comment