.

.

.

.

Wednesday

WAZIRI NAPE MGENI RASMI TAMASHA LA REJOYCE SEPTEMBA 16,2022

WAZIRI wa Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Mnauye anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika tamasha la Kusifu na Kuabudu la Rejoice litakalofanyika Septemba 16,2022 katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar Es Salaam.

Akizungumza na waandishi habari leo Septemba 13, mlezi wa kwaya ya Moravian Efatha, Yona sonelo amesema maandalizi yamefikia Asilimia 95 Katika kuelekea siku ya tamasha hilo huku wanakwaya mbalimbali wameshathibitisha kuhudhuria tamasha hilo.

"Siku ya Tamasha tarehe 16 ya mwezi wa tisa Mgeni Rasmi atakuwa ni waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye"

Amesema Wanakwaya wa kwaya moravian efatha choir, watawakutanisha wasanii mbalimbali wa nyimbo za injili kutoka Afrika uwanjani hapo.

Amesema siku ya kesho kwaya Moravian itaanza mazoezi ya mitambo ya sauti na siku ya alhamisi kwaya ambazo zimealikwa watafanya mazoezi ikiwemo kwaya ya joyous celebration kutoka Afrika kusini.

Ameongezea kuwa tamasha la rejoice litaanza kuanzia saa 11 jioni na waimbaji wataanza kuimba mpaka alfajiri ya Tarehe 17 siku ya jumamosi.

Kwa upande wa Usalama siku ya tamasha jeshi la polisi limejipanga kuhakikisha watu wanakuwa salama muda wote wa tamasha hilo.

Aidha amesema tiketi Bado zinapatikana Katika app ya 'NILIPE' ambazo zinaanzi VIP shilingi milioni moja, laki tano, laki moja, Elfu hamsini na elfu ishirini kwa kawaida.

"Tunawakaribisha watanzania wote Katika Tamasha la kuombea Nchi yetu ya Tanzania na Kwa wengine wanaotaka kununua tiketi uwanjani pia zitapatikana" Amasema Yona sonelo.



Mlezi wa Efatha Moravian kwaya ambaye ndiye muandaaji wa Tamasha la muziki wa Injili Yona Sonero Amesema ulinzi kwenye Tamasha hilo la Rejoice utakuwa ni wa uhakika na amewataka wananchi wafike bila kukosa,

Amesema kuwa wao kama waandaaji wameshafanya mazungumzo na vyombo mbalimbali vya Ulinzi ili kulifanukisha Hilo kwa asilimia mia moja,

Aidha amesema kuwa Kwaya zote maarufu Tanzania zitakuwepo.

Monday

AMDT YAWATAKA WAKULIMA WA ALIZETI MKOANI MANYARA KUCHANGAMKIA FURSA

Kaimu Katibu tawala mkoa wa Manyara,Anza Amen Ndosa akizungumza na Wajumbe wa Bodi ya Taasisi ya kuendeleza Mifumo ya Kimasoko ya Kilimo Tanzania (AMDT) walipotembelea ofisi ya mkuu wa mkoa huo kwa lengo la kuangalia namna AMDT inawezesha wakulima wa Alizeti kupitia miradi yake..kulia kwake ni Afisa Kilimo wa mkoa huo,Norbert Emmily .
Mkurugenzi Mtendaji  wa taasisi ya  Taasisi ya kuendeleza Mifumo ya Kimasoko ya Kilimo Tanzania (AMDT) ,Michael Kairumba akitoa taarifa kwa Wajumbe wa Bodi ya Taasisi hiyo namna ambavyo AMDT imekuwa ikiwawezesha wakulima wa zao la Alizeti kupitia miradi yake.
Afisa Kilimo mkoa wa Manyara ,Norbert Emmily akitoa taarifa kuhusu kilimo cha zao la Alizeti katika mkoa huo kwa Wajumbe wa Bodi ya  Taasisi ya kuendeleza Mifumo ya Kimasoko ya Kilimo Tanzania (AMDT) walipotembelea ofisi ya mkuu wa mkoa huo.
Mkurugenzi wa kampuni ya Quality Food Product (QFP) Sherry Woodring ambaye ni Mdau wa Taasisi ya kuendeleza Mifumo ya Kimasoko ya Kilimo Tanzania (AMDT) akitoa taarifa mbele ya Wajumbe wa Bodi ya taasisi hiyo kuhusu zao la Alizeti katika mkoa wa Manyara .
Mkurugenzi wa kampuni ya Quality Food Product (QFP) Sherry Woodring ambaye ni Mdau wa Taasisi ya kuendeleza Mifumo ya Kimasoko ya Kilimo Tanzania (AMDT) akitoa maelezo kwa  Wajumbe wa Bodi ya taasisi hiyo walipotembelea kiwanda cha kukamulia Alizeti kilichopo mkoani Manyara.
Sehemu ya Mitambo iliyopo katika kiwanda cha Kukamulia Alizeti kilichopo mkoani Manyara.
Magunia ya Alizeti yakiwa katika kiwanda cha kukamua Alizeti cha Agro 
Meneja Mradi wa Alizeti kutoka  Taasisi ya kuendeleza Mifumo ya Kimasoko ya Kilimo Tanzania (AMDT) Martin Mgallah akizungumza wakati Wajumbe wa Bodi ya taasisi hiyo walipowatembelea wakulima wa zao la Alizeti katika kijiji cha Mwada mkoani Manyara.
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii .
Babati Manyara.

TAASISI ya Kuendeleza Mifumo ya Kimasoko ya Kilimo- Tanzania (AMDT), imewataka wakulima wa zao la Alizeti mkoani Manyara kuachana na kilimo cha mazoea cha zao hilo na badala yake waelekeze nguvu katika kilimo cha kibiashara kwa kutumia pembejeo bora hasa mbegu na kufuata mbinu bora za ugani ili kuongeza tija kwenye mavuno na hivyo kukuza vipato vyao.

Hayo yamebainishwa na Meneja Mradi wa Alizeti unaosimamiwa na Taasisi ya AMDT, Martin Mgallah wakati wa ziara ya wajumbe wa bodi wa taasisi hiyo waliyoifanya hivi karibuni mkoani Manyara.
Katika ziara hiyo iliyokuwa na lengo la kujifunza na kuona mafanikio pamoja na changamoto za utekelezwaji wa mradi wa kilimo cha Alizeti kwa wakulima wa Mkoa wa Manyara, Bwana Mgallah alisema toka kuanzishwa kwa mradi huo, pamekuwepo na mwitikio chanya kutoka kwa wakulima wengi kushawishika kujikita kwenye kilimo cha zao la Alizeti.

Hata hivyo Bwana Mgallah ameongeza kuwa licha ya mapokeo chanya bado hitaji la zao la Alizeti kwa Mkoa wa Manyara ni kubwa na hivyo kufanya soko la mazao yatokananyo na alizeti kuwa kubwa ndani ya mkoa huo na mikoa mingine.

“Niwatoe hofu wakulima na hasa wanaoanza kulima zao hili kutoogopa kwani soko lake ni kubwa hapa Manyara lakini hata nje ya mkoa, masoko ni ya uhakika, Sisi kama AMDT tumedhamiria kutoa elimu kwa wakulima, kuwaunganisha na watoa huduma za msingi kwa kilimo na kuwasaidia kupata mbegu bora zililizoboreshwa zitakazo wawezesha kupata mazao kwa wingi,”alisema.

Mgallah amesema  iwapo wakulima watazingatia maelekezo ya wataalamu na matumizi ya mbegu bora basi Tanzania inaweza kuondokana na tatizo la uagizaji mkubwa wa mafuta ya kula kutoka nje ya nchi, ambapo takwimu zinaonyesha zaidi ya asilimia 60% ya mafuta hayo huagizwa toka nje ya nchi.

Kwa upande wake Kaimu Katibu tawala wa mkoa wa Manyara Anza Amen Ndossa amesema katika mkoa wa Manyara zao la Alizeti ni moja kati ya mazao ya biashara ya kimkakati ambayo mkoa huo umekuwa ukihamasisha wakulima kujihusisha nao, kutokana na ardhi ya eneo lao kuruhusu kusitawi kwa zao hilo.

“Kilimo cha Alizeti ni moja kati ya mazao ya biashara ambayo mkoa umekuwa ukihamasisha wakulima wetu kujihusisha nayo, Tunatambua mchango wake katika kuinua hali za Maisha za wananchi wetu, na ndio maana ujio wa wadau kama AMDT na QFP kwetu ni faraja maana mwisho wa siku utamsaidia mkulima wa hali ya chini kuweza kulima kwa tija na kuweza kujikwamua kiuchumi” Alisema Ndosa.

Kwa Upande wake Afisa kilimo wa Mkoa wa Manyara Bwana Norbert Emmily amesema toka kuanza rasmi kwa kilimo cha Alizeti mwaka 2000, wakulima wengi wamekuwa wakihamasika kujihusisha na kilimo hicho huku akitaja changamoto ya uhaba wa mbegu bora za Alizeti kuwa ni kikwazo kutokana na ukweli kwamba wakulima wengi wanatumia mbegu za asili, ambazo utoaji wake wa mafuta umetajwa kuwa wa chini ukilinganisha na mbegu Chotara.

Mkoa wa Manyara kwa sasa kwa mujibu wa takwimu za uzalishaji wa zao hilo zinaonyesha kumekuwepo na ongezeko kubwa la tija kwa wakulima na hasa katika mavuno ambapo kwa sasa mkulima anapata wastani wa gunia sita mpaka gunia nane ukilinganisha na gunia mbili mpaka tatu mpaka nne kwa eka mnamo mwaka 2006.

Tuesday

TCRA YASISITIZA MATUMIZI SAHIHI NA SALAMA YA MITANDAO NCHINI

Katika kupambana na makosa ya uhalifu wa kimtandao nchini TCRA kwa kushirikiana na kampuni ya Kingdom Heritage ilifanya semina kwa vijana yenye lengo la kuwajengea uelewa wa namna nzuri ya matumizi na usalama Mtandao.

Semina hiyo ilifanyika mwishoni mwaka wiki iliyopita katika ukumbi wa Buni Hub tume ya Sayansi Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na vijana kutoka vyuo na taasisi mbalimbali za serikali na binafsi.

Mwanansheria mwandamizi kutoka TCRA, Dk Philip Filikunjombe alipokuwa akizungumza katika warsha hiyo alisema  kulingana na ukuaji wa miundombinu ya TEHAMA inakuwa kwa kasi na kusababisha matokeo chanya na hasi katika jamii zetu
“Katika majira haya ya maendeleo ya TEHAMA waharifu wanatumia mwanya huo kufanya uharifu katika mifumo mbali mbalimbali ya Kompyuta hivyo tunatakakiwa kuwa makini kwa watumiaji wa mitandao na wadau wa TEHAMA nchini,” alisema Dk Filikunjombe.

Alisema kama TCRA wanazidi kusisitiza kuhusu matumizi sahihi na salama ya mitandao tena yenye maadili ili kupunguza uhalifu huo, Kwa kushirikiana na Jeshi la polisi kitengo cha uhalifu wa kimtandao.

Mwanzilishi wa Jamii Forums na muwasilishaji mada katika warsha hiyo, Maxence Melo alizungumzia fursa mbalimbali zinazopatikana katika mitandao na miundombinu ya TEHAMA kwa kuwasihi vijana waliokuwa hapo kuwa wabunifu katika majira haya na kuja na mifumo suluhisho itakayoweza kutumika katika jamii zetu.

“Serikali pia kupitia wizara au mamlaka zinazohusika kusapoti juhudi za vijana wabunifu katika TEHAMA  kwa miundombinu na kanuni na taratibu rafiki ili waweze kujifanikisha katika ubunifu wao mpaka kijipatia kipato binafsi na taifa zima kwa ujumla.” Alisema Melo.

Mtaalamu wa masuala ya ulinzi katika mfumo ya Kompyuta na TEHAMA nchini kutoka Kampuni ya Kabolik, Robert Matafu alizungumzia  namna ya kujilinda dhidi ya mashambulizi ya kimtandao na kuwa salama mtandaoni.

“Nchi nyingi za Afrika tunakosa uelewa wa maarifa ya kujilinda na mashambulizi ya kimtandao na kupelekea kupata hasara sana katika taasisi au watu binafsi kutokana na mashambulizi hayo,” alisema Matafu.

Aliongeza “Takwimu zinaonyesha taasisi nyingi afrika na Tanzania tukiwepo hatuwekezi vya kutosha katika mifumo ya kiulinzi na usalama mtandao,kwa kufanya hivyo tunaongeza asilimia kubwa za kupata mashambulizi ya kimtandao katika tasisi zetu,” alisema.

Awali, Mkurugenzi wa Kampuni ya Kingdom Heritage waandaaji wa semina hiyo Tunu  Bashemela alisema wao kwa sehemu yao wanaunga mkono juhudi za serikali kupitia TCRA katika kupambana na makosa ya uharifu wa kimtandao kwa kutoa elimu kwa umma hasa vijana ambao ndio rika linalotumia sana mitandao.

“Ili kujua matumizi sahihi na salama vijana mliopo hapa lazima mtambue kuwa sheria ya makosa ya uhalifu wa kimtandao ipo na inafanya kazi lazima tuheshimu na kutii vitu inavyotuzuia kufanya bali tutumie mitandao kwa namna za ubunifu zenye kutuletea fedha na kujiingizia kipato,” alisema Bashemela.



Mwanansheria mwandamizi kutoka TCRA, Dk Philip Filikunjombe

Mwanzilishi wa Jamii Forums mmoja kati ya wawasilishaji mada katika warsha hiyo, Maxence Melo
Mkurugenzi wa Kampuni ya Kingdom Heritage ambao ndio waandaaji wa semina hiyo Tunu  Bashemela
Vijana mbalimbali watumiaji wa mitandao na wadau wa TEHAMA waliohudhulia semina hiyo wakifuatilia kwa makini







Mtaalamu na Mshauri wa masuala ya ulinzi katika mfumo ya kompyuta na TEHAMA nchini kutoka Kampuni ya Kabolik, Robert Matafu katika mjadala na nini kifanyike ili kupunguza na kukomesha matukio ya uhalifu wa mtandao nchini.
  Mtendaji Mkuu wa tzNIC  Abibu Ntahigiye katika mjadala wa katika mjadala na nini kifanyike ili kupunguza na kukomesha matukio ya uhalifu wa mtandao nchini.
Mwanzilishi wa Jamii Forums katika mjadala na nini kifanyike ili kupunguza na kukomesha matukio ya uhalifu wa mtandao nchini.