.

.

.

.

Monday

Kanisa lawataka Wachungaji wajiuzulu Chadema

Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kusini ambaye pia ni Mchungaji wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT), Joseph Matare amejiuzulu nafasi yake hiyo kutokana na kanisa lake kuwataka wachungaji wake ambao ni viongozi wa vyama vya siasa kuachana na nafasi zao za kisiasa.

Joseph Matare akizungumza na waandishi wa habari mjini Songea amesema kuwa ameamua kujiuzulu nafasi yake ya uongozi wa Chadema Kanda ya Kusini inayojumuisha mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma baada ya kanisa lake katika mkutano wake wa kanda kuagiza wachungaji wake ambao ni viongozi wa siasa kuachia nafasi zao na badala yake wasimamie kazi ya Mungu katika makanisa yao.

“Kufuatia maagizo ya mkutano huo wa kanisa uliofanyika Njombe nimeamua kutii... nimeamua kujiuzulu na katibu wangu mkuu, Dk Willibrod Slaa nilimjulisha tangu tarehe 4 Juni mwaka huu,” alisema Matare katika taarifa yake ya kujiuzulu.

Amefafanua kuwa muda wa viongozi wa kanda ulikuwa ni wa muda na wa mpito hadi uchaguzi wa kanda utakapopita ambao ulipaswa kufanyika Juni 2014 na kwamba muda umeongezwa hivyo ameona aheshimu maagizo yaliyomweka madarakani.

Hata hivyo, Matare anasema kuwa anawatia moyo makamanda wote wa Chadema waliobaki kuendelea kupigania nchi ili iondokane na uovu unaotendeka sasa na kwamba Mungu atakuwa nao wale wote wanaotafuta haki kwa ajili ya wananchi walio

Source:Mwananchi

No comments:

Post a Comment