.

.

.

.

Tuesday

Pata Kutiwa Moyo na Ushuhuda wa Neema alivyoponywa UKIMWI

Tunampa Mungu utukufu wote kwa Ushuhuda wa uponyaji wa UKIMWI jinsi alivyodhihirisha nguvu za uponyaji wake, piakutuwezesha kushuhudia zaidi ya watu 50 wakiponywa UKIMWI katika huduma yetu. Nina imani kwamba shuhuda hizi zitaweza kusaidia kuinua imani, ya wale wanaomwamini Mungu kwa ajili ya uponyaji wa magonjwa yasiyo na tiba kama UKIMWI na kutoa changamoto kwa watumishi wa Mungu kuwasaidia wagonjwa kupokea uponyaji wao kwa kuhubiri Neno la imani na uponyaji.

Neema aliponywa na ugonjwa ambao kwa madaktari hauna dawa wala tiba yaani UKIMWI Agosti 2012 kwa msaada wa mafundisho ya uponyaji aliyoyapata kwa Mchungaji Prosper Ntepa mwaka 2006 hadi 2008 baada ya kuishi na virusi vya UKIMWI kwa takribani miaka sita. Wakati watu wengi wamekata tamaa kwa sababu ya taarifa ya madaktari inayosema UKIMWI hauna dawa wala tiba kuna dawa imegunduliwa katika maabara za kiroho na kitabu kinachoitwa Biblia ambayo inaanza kumponya mgonjwa kuanzia katika mizizi ya roho yake na kufisha vidudu vya UKIMWI. Mafundisho ya ugunduzi wa dawa hii kiboko yameonekana kuleta matokeo katika huduma ya mchungaji Prosper Ntepa, ambapo kuna taarifa zinazosema watu zaidi 50 wameponywa UKIMWI kwa uthibitisho wa madaktari. Dada Neema ni mojawapo wa watu waliopata neema ya kuponywa kwa njia ya imani katika dawa ya Neno la Mungu ambayo imethibitika kuleta matokeo ya ajabu kwa wale wanaoiamini na kuimeza kwa umakini na kufuata masharti yake. 

Mchungaji Prosper Ntepa wa The Oasis of Healing Ministries
Ni muhimu kukumbuka kwamba kuwa na UKIMWI siyo tatizo bali ni mtazamo unaokuwa nao juu ya UKIMWI ndio tatizo kubwa kuliko UKIMWI wenyewe. Kwa maneno mengine, kuwa na tatizo sio tatizo bali ni mtazamo unaokuwa nao juu ya tatizo ndio tatizo kubwa kuliko tatizo lenyewe. Mmoja ya watu waliokuwa wakimwamini Mungu kwa ajili ya uponyaj aliwahi kusema kwamba, “Watu wengi walioathirika na UKIMWI wameathirika katika ufahamu na mawazo yao.” Jambo hili nimeliona kuwa kweli katika uzoefu wa kufanya ushauri kwa mamia ya watu walioathirika na UKIMWI. Ufahamu au mawazo yanaathirika kwa sababu ya ripoti inayosema UKIMWI hauna dawa wala tiba. Kwa hiyo mtu akipata ugonjwa huu anaathirika katika ufahamu na mawazo yake kiasi kwamba mtazamo wake unakuwa ni hasi au mtazamo mbaya. Katika akili mtu huyu anajaa mawazo yanayoamini katika hali ya kutokuwezekana au hali ya kutokuamini.
Sauti ya mawazo ya kutokuamini inaanza kumpa taarifa mtu kwamba hana haja ya kumwamini Mungu kwa ajili ya uponyaji au muujiza wake. Hatimaye anatawaliwa na mawazo ya kufa zaidi kuliko kupona na kuishi.

Dada Neema alizaliwa Itigi akiwa mtoto wa pili katika familia ya watoto wawili. Baba na mama ni Waislamu. Alioana na mume wake wa sasa Novemba 2003. Wamejaliwa kupata mtoto mmoja wa kike anayeitwa Abighail katika ndoa yao ambaye alizaliwa tarehe 27 Mei 2009.  Abighail alizaliwa wakati mama yake akiwa ameathirika na UKIMWI. Wakati wanaoana hawakupima afya kwa habari ya UKIMWI.
  
 Je, uliambukizwaje virusi vya UKIMWI?
 Ninashindwa kuelewa jinsi nilivyopata maambukizo ya UKIMWI. Niliwahi kuolewa na kuachika kabla ya kukutana na mume wangu wa sasa. Mume wangu wa sasa alifiwa na mke wake kwanza. Tumeshindwa kujua kwamba tatizo la maambukizo lilitoka kwangu au kwa mume wangu. Taarifa nilizozipata ni kwamba mke wa kwanza wa mume wangu alifariki Machi 2003 kwa ugonjwa wa maralia na kuchanganyikiwa. Tatizo ni kwamba hatukupima afya zetu wakati tunaingia katika ndoa.

Je ulijuaje kama umeathirika na virusi vya UKIMWI?
 Mwishoni mwa 2006 nilipima katika hospitali ya Amana na kukutwa na virusi vya UKIMWI. Baadaye nikapima tena sehemu nyingine mbili ambako walithibitisha pia kwamba nimeathirika na UKIMWI. Vile vile mume wangu alipimwa na kukutwa kwamba alikuwa naye ana virusi vya UKIMWI.   
Je, ulikuwa na dalili gani za magonjwa nyemelezi?
 Nilikuwa na dalili nyingi za magonjwa nyemelezi ya UKIMWI. Dalili hizi ni pamoja na homa za mara kwa mara, malaria, kuwashwa sehemu za siri na kuvimba mwili. Pamoja na mwili wangu kubadilika rangi ya weupe na kuwa mweusi kama mkaa nikajikuta nikawa na vidonda mdomoni kiasi cha kuanza kutoa harufu. Kuna wakati ambao niliumwa sana na kusababisha kupungukiwa na damu kiasi cha kufikia tatu nukta nne. Pia nikapata mkanda wa jeshi kwa muda wa miezi mitatu ambao ulinitesa sana.

Uliokoka lini?
Nilikuwa mwislamu kwa  sababu baba na mama ni waislamu. Nilikuwa nina tabia ya kupenda kusikiliza kanda za nyimbo za Kikristo. Niliokoka Julai 2003 kupitia vipindi vya Neno la Mungu kupitia redio za Kikristo za hapa Dar es Salaam. Baada ya kuokoka nilisali makanisa mbalimbali ya Kipentekoste. Kuna wakati nilianza kusali katika kanisa la Full Gospel Bible Fellowship la Mwenge, ambako sikukaa zaidi ya mwezi mmoja. Baada ya kuokoka nilibatizwa kwa maji mengi katika kanisa la Askofu Sylvester Gamanywa. Mume wangu aliponywa ugonjwa sugu wa fangasi iliyomsumbua kwa miaka takribani miaka kumi na nne. Baadaye mimi na mume wangu tulihamia katika kanisa la The Oasis of Healing Ministries, baada ya kusikia mafundisho kupitia Praise Power Radio. Tulijiunga na huduma hii kuanzia mwishoni mwa 2006. Tulipokuja katika ukumbi wa Mhasibu house tulisikia ushuhuda wa dada Hellen ambaye aliponywa UKIMWI katika wiki ya kwanza aliyokuja katika maombezi wakati ni mjamzito kabla ya kuolewa. Tulisikia shuhuda za watu wengine ambao pia walikuwa wameponywa UKIMWI katika huduma ya mchungaji Prosper Ntepa. Matokeo yake tulitiwa moyo sana.

Je, ulipima mara ngapi kuthibitisha kwamba una virusi vya UKIMWI? 
Nilipima mara tatu kuthibitisha kwamba nina maambukizo ya UKIMWI. Mara ya tatu nilipima katika kituo katika afya kilichoko Mbagala.

Je, uliponywaje ugonjwa wa UKIMWI? Ni vitu gani vilikusaidia kupokea uponyaji wa UKIMWI?
 Nilikuwa mshirika katika kanisa The Oasis of Healing Ministries kuanzia mwishoni mwaka 2006 mpaka mwishoni mwa 2008. Baada ya hapo tukawa tumehamia Sanya Juu, Kilimanjaro. Kuna mchungaji mmoja ambaye alikuja kufungua kanisa Sanya Juu tukaongozwa kushirikiana naye katika kazi ya Mungu. Kama shukrani kwa Mungu kwa yale ambayo Mungu alitufanyia mume wangu aliamua kutoa sehemu ya kiwanja chake cha urithi kwa ajili ya kujenga kanisa pale Sanya Juu. Nilipata uja uzito mwishoni 2008. Tulipata mtoto wa kike ambaye tulimpa jina la Abighail ambaye alizaliwa kabla ya muda wake tarehe 27 Mei 2009 akiwa na miezi saba. Mwaka 2008 nikiwa na mimba nilipimwa damu na kugundulika kuwa bado nilikuwa ninaishi na virusi vya UKIMWI. Lakini bado sikukata tamaa katika imani. Niliendelea kumwamini Mungu na Neno lake bila kutetereka. Hatimaye uponyaji wangu ulikuja kuthibitika Agosti 2012 baada ya kuvumilia na kusimama katika Neno la Mungu kwa takribani miaka mitano na nusu. Uponyaji wangu ulikuja kugundulika wakati nilipoumwa sana malaria nikalazimika kulazwa katika hospitali ya Kibongoto. Madaktari wakanishauri nilipokuwa ninatibiwa malaria nipime pia damu kuangalia kama bado nina UKIMWI. Baada ya madaktari kunipima damu wakashangaa kugundua kuwa nilikuwa sina maambikizo ya UKIMWI. Jambo hili liliwapa mshangao mkubwa kwa sababu walikuwa wamewahi kunipima na kunikuta na maambukizo ya UKIMWI. Huko nyuma wakati nilipokuwa na dalili nyemelezi za UKIMWI madaktari walikuwa wamenipima mara kadha na kunikuta nina virusi vya UKIMWI. Kwa maneno mengine, baadhi ya madaktari walikuwa wanajua kwamba nilikuwa nimeathirika na virusi vya UKIMWI. Madaktari hao walishangaa sana kunikuta nikiwa na majibu tofauti na matarajio yao ya awali. Wakaanza kunihoji maswali kwamba imekuwaje hali yangu imebadilika ghafla hivi na kutokuwa na virusi vya UKIMWI. Nikawajibu kwamba Bwana Yesu ameniponya na UKIMWI. Nikawapa ushuhuda jinsi nilivyoishi katika imani ya kulitegemea Neno la Mungu. Nikawasimulia jinsi nilivyokuwa ninakiri au kutamka  mistari ya uponyaji mara kwa mara. Nikawashauri kwamba kama wana mashaka na jambo hili basi wawasiliane na Mchungaji Prosper Ntepa kanisa la The Oasis of Healing Ministries, Ubungo ili wapate ushahidi zaidi wa uponyaji wa UKIMWI.

Matokeo yake madaktari wale wakarudi tena kunipima kipimo cha CD4 yaani kiwango cha kinga yangu. Baada ya kunipima walishtuka kugundua kuwa CD4 au kiwango cha kinga za mwili wangu zikiwa zimeongezeka sana yaani kiwango cha mtu ambaye hana virusi vya UKIMWI. Kiwango cha kinga zangu zilipanda sana tofauti na kiwango cha awali wakati nikiwa ninaishi na virusi vya UKIMWI. Pia waliporudia kunipima kipimo cha kubainisha kama nimeathirika na UKIMWI au sina maambukizo ya UKIMWI. Wakapima tena damu na kukuta sina maambukizo ya UKIMWI yaani HIV negative. Kwa hiyo madaktari walinipima mara tatu yaani vipimo viwili vilivyoonyesha sina UKIMWI au HIV Negative na kipimo kingine cha kupima CD4.

Magonjwa nyemelezi yalipungua baada ya kujifungua mtoto wangu Abighail kuanzia 2009. Niliacha kutumia dawa za kurefusha maisha kuanzia Juni 2009. Badala yake nilikuwa ninatumia dawa ya Neno la Mungu yaani kuzitamka ahadi na kweli za uponyaji. Nilisimama katika ahadi na kweli za uponyaji mbalimbali ambazo zilinisaidia kuniimarisha kiimani. Baadhi ya mistari niliyokuwa ninaisimamia kwa njia ya kuikiri na kuitamka ni hii ifuatayo: Niliamini kwamba Mungu analitumia Neno kama dawa ya kuniponya mimi. Zaburi 107:20, “Hulituma neno lake, huwaponya, huwatoa katika maangamizo yao.” 1 Petro 2:24, “Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa.” Nilikuwa nanakiri kwamba kwa kupigwa Yesu nimepona na niko huru na UKIMWI.

Mathayo 8:17, “Ili litimie lile neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema, mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu na kuyachukua magonjwa yetu.” Katika Mathayo 8:17 nilikuwa ninakiri kwamba Yesu alitwaa udhaifu wangu na kuyachukua magonjwa yangu. Kutoka 15:26, “Akawaambia, Kwamba utaisikiza kwa bidii sauti ya Bwana, Mungu wako, na kuyafanya yaliyoelekea mbele zake, na kutega masikio usikie maagizo yake, na kuzishika amri zake, mimi sitatia juu yako maradhi yo yote niliyowatia Wamisri; kwa kuwa Mimi ndimi Bwana nikuponyaye.”
Yohana 10:10, “Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.”Nilimtambua Ibilisi kama mwizi wa afya yangu lakini Yesu alikuja ili niwe na uzima na niwe nao tele. Nilianza kuamini katika hali ya kutokufa kabla ya wakati wangu. Ayubu 5:26 ilinitia moyo, “Utafika kaburini mwenye umri mtimilifu, kama mganda wa ngano ulivyo wakati wake.”

 Katika mchakato huu wa kulipanda Neno la Mungu kama dawa kwa ajili ya uponyaji nilifikia hatua ya kukariri mistari mingi. Mimi na mume wangu tuligundua kwamba Neno likiwa katika Biblia ni Andiko lakini linapokuwa ndani ya roho yako linakuwa Neno lililo hai. Biblia inasema katika 2 Wakorintho 3:6, “Naye ndiye aliyetutosheleza kuwa wahudumu wa agano jipya; si wa andiko, bali wa roho; kwa maana andiko huua, bali roho huhuisha.” (Kwa maneno mengine, walitofautisha logos yaani Neno la Mungu la jumla lisemwalo na rhema yaani Neno la Mungu maalum au la ufunuo linasema kitu sasa. Watu wengine wanashindwa kujenga imani ya uponyaji pamoja na ukweli kwamba wanalijua Neno kwa akili zao lakini hajafikia hatua ya kuwa na Neno lililofunuliwa katika roho zao)


Unamshauri nini mtu anayemwamini Mungu kwa ajili ya uponyaji wa UKIMWI na unaonekana kuchelewa?
Ningependa kushauri mambo matatu yafuatayo. Kwanza, ninashauri wazingatie kumkubali na kumwishia Mungu. Pili, ninawashauri walikubali na kulitafuta Neno kwa bidii. Tatu, ninashauri wasikate tamaa katika kumwamini Mungu. Waendelee kukiri mistari ya uponyaji hadi uponyaji wao utakapodhihirika. Nina imani wataweza kupona kama mimi nilivyopona.


  Je, ulikutana na hali zozote za kukatisha tamaa?

Ni kweli nilikutana na hali za kukatisha tamaa katika mchakato wa kufikia kupokea uponyaji wangu. Halikuwa jambo rahisi kuendelea kumwamini Mungu. Sikuwa na roho ya kuogopa kufa. Nilikuwa ninasikia sauti ndani yangu inayosema, “Unasimama katika Neno la Mungu lakini hakuna mabadiliko yoyote katika mwili wako. Unaomba kila siku hupati uponyaji wako. Wewe utaishia kufa tu. Huwezi kupona UKIMWI.” Nikawa ninakataa kukubaliana na maneno haya kutoka kwa adui shetani. Nilikuwa ninaipinga sauti hiyo kwa jina la Yesu.



Kwa upande mwingine nilikuwa ninasikia sauti inayosema “Umekwisha kupona UKIMWI. Wewe ni mzima.” Sauti ya adui ilikuwa inanihubiri kwamba nitakufa wakati sauti ya Mungu ilikuwa inanithibitishia kuhusu kupona. Nikaamua kuifuata sauti chanya iliyosema kwamba nimepona. Mwishowe nikaanza kujiona na kukubaliana juu ya uponyaji wangu. Nikaanza kumshukuru Mungu kwa ajili ya uponyaji wangu. Nikawa ninasema, “Asante Yesu Kristo kwa kuniponya UKIMWI. Asante Yesu Kristo kwa sababu wewe ni mponyaji wangu.” Kwa maneno mengine niliacha kukazana kuomba dua za Mungu kuniponya UKIMWI na kuanza kumshukuru Mungu kwa ajili ya uponyaji wangu kana kwamba tayari ulikuwa umefanyika halisi. 


Je, kuna mtu yeyote aliyeponywa UKIMWI ambaye alikutia moyo katika kumwamini Mungu?
Michael aliyeponywa na UKIMWI 2006 baada ya kuishi na UKIMWI kwa miaka mitano alitutia sana moyo mimi na mume wangu. Niliposikia ushuhuda wa kuponywa kwake virusi vya UKIMWI nilifarijika sana kwamba kwa Mungu hakuna ugonjwa usioweza kutibika. Kuna wakati Michael alikuja nyumbani kumwona mume wangu wakati anaumwa.

 Una washauri nini watu wanaotaka kupokea uponyaji wa UKIMWI?
 Ninataka kushauri mambo manne yafuatayo: Kwanza, ninawashauri wanaotaka kupokea uponyaji wa UKIMWI waishi maisha matakatifu. Kuishi katika dhambi kama za uzinzi kunaweza kumzuia mtu kupokea uponyaji wake. Pili, usiwe na shauku kwamba ukipona ugonjwa wa UKIMWI utajitoa kufanya maovu. Ninashauri mtu atengeneze shauku ya kumtumikia na kumwishia Mungu. Tatu, ninashauri mtu anayetaka kuponywa UKIMWI akatae kuathirika kwa ufahamu au mawazo yake. Unaweza kuathirika na UKIMWI lakini ukakataa kuathirika kimawazo kwa njia ya kuwa mtazamo chanya. Mungu anaweza kufanya njia pasipo na njia. Asikubali sauti ya milango mitano ya maarifa inayotumia kuona, kusikia, kuonja, kugusa na kushika. Ni jambo la muhimu kuipinga sauti ya shetani inayowasiliana katika mawazo yako. Nne, ni muhimu kujifunza kunukuu na kukiri Neno linavyosema katika hali ya ugonjwa wako kwa kulitamka. Nina ushahidi wa Neno la Mungu linavyosema. Yeremia 33:6, “Tazama, nitauletea afya na kupona, nami nitawaponya; nami nitawafunulia wingi wa amani na kweli.”

Je, kuna mtu yeyote ambaye ameponywa UKIMWI kwa msaada wako?
Tulipokuwa Sanya Juu, Kilimanjaro mume wangu alianza kufundisha Neno la Mungu katika kanisa moja na kufanya huduma ya kuombea wagonjwa. Watu walianza kuja kuombewa magonjwa mbalimbali na wakawa wanapona. Mimi na mume wangu tulimsaidia mama mmoja ambaye yeye na mume wake walikuwa wameathirika na UKIMWI. Huyu mama alianza kusikiliza mafundisho ya Neno la Mungu, ambayo mume wangu alikuwa anafundisha. Ilikuwa ni Oktoba 2012. Tulimfundisha kukiri mistari ya uponyaji ambayo tulijifunza kwa Mchungaji Prosper Ntepa. Huyu mama alikuwa amepima mara nne kwamba ana virusi vya UKIMWI. Wakampima na kukuta hana virusi vya UKIMWI. Mama huyu aliambiwa arudi tena Januari 2013 baada ya miezi mitatu. 

No comments:

Post a Comment