.

.

.

.

Monday

UKO NDANI YA MUNGU NA YEYE YUKO NDANI YAKO – Huna sababu ya kuhofu chochote

Wapendwa, kama watoto wa Mungu, tusikubali kuyumbishwayumbishwa ama kubabaishwa na chochote kila katika maisha haya. Tuelewe ya kuwa uzima wetu na maisha yetu vimo ndani ya Mungu – Yes – ndani ya Mungu Mwenye Enzi yote Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na tunaishi kwa uweza wake, Mtume Paulo alikuwa na mengi ya kusema kuhusu hili, ngoja niorodheshe japo machache. 
 
Paulo alisema ndani yake yeye tunaishi, tunakwenda, na kuwa na uhai wetu. (Matendo 17:28) Na mahali pengine akasema tulikufa na sasa uhai wetu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu (Wakolosai 3:3) Na kama hiyo haitoshi tumekumbushwa na Mtume Paulo mara kadhaa ya kuwa baada ya Kristo Yesu kutufia pale msalabani na kutupatanisha na Baba basi hii miili yetu inafanyika Hekalu la Roho Mtakatifu 
tunapomwamini Yesu (1 Wakorintho 6:19). Mtume Paulo pia alifikia kusema hivi:
20 Nimesulibiwa pamoja na Kristo; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu; na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda, akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu. - Wagalatia 2:20 SUV 
 
Tumeungamanishwa na Mungu na kuwa roho moja naye...we are no longer separated from God! Wow!
17 Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye. – 1 Wakorintho 6:17 SUV
 
Nimekakumbuka kale kawimbo ketu kazuri... “Siyo mimi ninayeishi bali Kristo ndani yangu,...”
Natamani tunapokaimbaga tuimbe tukitafakari kweli hii ya kwamba Mungu wa Milele yote, Mungu Mwenye Enzi na Mamlaka yote, Muumba wa Mbingu na Nchi na vyote vinavyoonekana na visivyoonekana, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, pamoja na Kristo Yesu mwenyewe wameweka makao ndani yetu - tusiishie kuimba kimazoeamazoea tu. 
 
Wapendwa yaani if we only knew the Treasure we have in these earthen vessels....if we only knew...
Mpendwa mtoto wa Mungu, amini na uelewe ya kuwa upo ndani ya Kristo na Yeye yupo ndani yako muda wote, 24/7, mithili ya Mzabibu na matawi yake, hata kama hisia zako zinagoma au mazingira yako hayaonekani kuwa hivyo....Hisia zetu hubadilikabadilika, mazingira yetu nayo vivyo hivyo, lakini lile asemalo Mungu limethibitika milele hivyo halibadiliki. 
 
Hivyo simama imara katika ufahamu huo na uyakabili maisha ukijua aliye ndani yako ni Mkuu kuliko aliye katika Dunia na wewe kama mtoto wake uliyezaliwa kwa Mbegu isiyoharibika ya Neno lake, amekushirikisha asili yake ya Kiungu ambayo inakupa hekima, maarifa, ufahamu na yote unayohitaji ili kuweza kuyakabili, kuyamudu na kuyaboresha maisha yako na ya wanaokuzunguka kwa utukufu wa Mungu.
Mpendwa, unayaweza mambo yote katika Kristo Yesu akutiaye nguvu! Chukua hatua…With Christ you can do all things
 
Somo na Patrick Kamera

No comments:

Post a Comment