.

.

.

.

Friday

Baba Mtakatifu aosha miguu ya waislamu

Mkuu wa kanisa katoliki duniani Papa Francis ameosha miguu ya wahamiaji waislamu mjini Rome katika tukio la unyenyekevu linaloambatana na itikadi ya kuanza kwa msimu wa Pasaka.

Papa Francis alitembela makao ya wahamiaji, mjini Roma na kuendesha misa ya kuanza kwa msimu wa pasaka.

Ziara yake katika kituo hicho cha kutathmini uhalali wa wahamiaji cha (Castelnuovo di Porto), inawadia huku uhasama na taharuki ikienea kote barani ulaya kuhusiana na kuwepo kwa wahamiaji waislamu hususan kufuatia mauaji ya Paris mwezi Novemba na ya hivi punde huko Brussels Ubelgiji.
Papa Francis alikashifu mauaji yaliyotokea Ufaransa na Ubelgiji akisema kuwa hizo ni njama za watu wenye kiu cha kumwaga damu ya binadamu.
Kiongozi huyo wa kanisa katoliki duniani alilaumu mtazamo wa watuhumiwa hao kuhusu maafa waliyosababisha.

Aidha papa mtakatifu aliwashauri watu wa dini tofauti duniani kuishi kwa amani.
''Haijalishi iwapo tunaimani tofauti la muhimu kwetu sote ni tuishi kwa amani sisi ni ndugu alisema papa mtakatifu.

Source bbc.com

No comments:

Post a Comment