Ili mfanyabiashara ama mzalishaji aweze kuuza bidhaa, ama huduma yake kwa
usalama na bila usumbufu anahitaji kuwa na alama ya ubora katika bidhaa yake (tbs).
Kwani alama hii ndio ikatayo thibitisha usalama na ubora wa bidhaa hiyo. Alama hii
hutolewa na shirika la viwango Tanzania kama moja ya skimu ya kudhibiti ubora wa
Ili mzalishaji aweze kuwa na alama ya ubora katika bidhaa yake anatakiwa kumiliki
leseni ya alama ya ubora kutoka shirika la viwango Tanzania (TBS). hivyo basi, zipo
hatua mbalimbali ambazo mzalishaji hupaswa kuzingatia kabla ya kupata leseni ya
kutumia alama ya ubora ya TBS kwenye bidhaa yake.
Hatua ya kwanza ni maombi ya uthibitishaji ubora ambayo hufanywa na mwombaji
kwenda kwa Mkurugenzi Mkuu wa shirika la viwango Tanzania kwa maandishi. Majibu
hutolewa yakielezea taratibu za kufuata na gharama zote zinazohitajika.
Majibu hayo huambatana na fomu maalum ambayo mwombaji huijaza na kuirudisha
TBS ikiwa na viambatanisho vifuatavyo: mtiririko wa uzalishaji wa bidhaa husika, mfumo
wa uongozi ukionyesha kitengo cha udhibiti ubora, orodha ya malighafi anazotumia na
mahali zinakotoka kwa kila bidhaa pamoja na ramani inayoelekeza jinsi ya kufika
kiwandani kwake.
Baada ya kutekeleza na kuwasilisha nyaraka hizo, tarehe ya kufanya ukaguzi wa awali
hupangwa. Izingatiwe kuwa mwenye kiwanda anatakiwa kuwa katika uzalishaji siku ya
kufanya ukaguzi wa awali.
Hatua inayofuata ni ukaguzi wa awali, ambayo ufanywa na wakaguzi wa TBS. ambapo
sampuli uchukuliwa na kupimwa ili kuona kama bidhaa inakidhi matakwa ya kiwango
husika. Mkaguzi huandaa taarifa kuhusu hali halisi ya kiwanda na mambo yanayostahili
kurekebishwa.
Hatua ya tatu ni upimaji wa sampuli zilizochukuliwa, na upimaji huo unafanyika katika
maabara za shirika la viwango Tanzania kwa kufuata kiwango husika. Baada ya kazi ya
upimaji kumalizika, ripoti hutolewa kwa mwombaji.
Hatua ya nne na ya mwisho ni utoaji wa leseni: uamuzi kuhusiana na kutoa ama
kutotoa leseni ya kutumia alama ya ubora hutegemea tu ripoti ya ukaguzi wa awali wa
kiwanda pamoja na ripoti ya maabara.
Kimsingi ripoti zote mbili zinatakiwa kuonyesha kwamba mazingira ya uzalishaji
kiwandani, mfumo wa uzalishaji na bidhaa iliyopimwa havina matatizo. Ikiwa sivyo basi
mzalishaji hutakiwa kufanya marekebisho na baadaye mkaguzi wa TBS hutumwa tena
na kuleta sampuli nyingine.
Vilevile, serikali imejaribu kutenga fungu kila mwaka kwa ajili ya wajasiriamali wadogo
na wa kati na kati ya hao wajasiriamali hao wanaweza samehewa kulipa ada yoyote
wanapoomba bidhaa zao kuthibitishwa ubora.
Hivyo basi, mjasiliamari ili kuweza kupata msamaha huo anatakiwa kupata barua ya
utambulisho kutoka ofisi ya SIDO iliyokaribu au chama cha wazalishaji mfano TAFOPA.
Taarifa fupi kutoka idara ya Afya iliyo karibu na mahali pa uzalishaji au cheti cha TFDA
kwa wale wanajihusisha na uzalishaji wa chakula huhitajika.
Muda wa alama ya leseni hiyo hudumu kwa mwaka mmoja. Na baada ya kupata leseni
ya kutumia alama ya ubora wanapaswa kutunza taarifa za uzalishaji na mauzo ambazo
zitahitajika kwa ajili ya ukaguzi wa baadae ukataofanywa na shirika.
Ili uendelee kudumu sokoni na kufanikiwa sana kibiashara alama hii ya ubora ni kitu
muhimu sana kwako mzalishaji na mteja pia.
usalama na bila usumbufu anahitaji kuwa na alama ya ubora katika bidhaa yake (tbs).
Kwani alama hii ndio ikatayo thibitisha usalama na ubora wa bidhaa hiyo. Alama hii
hutolewa na shirika la viwango Tanzania kama moja ya skimu ya kudhibiti ubora wa
Pastor,Adv Justine Kaleb |
Ili mzalishaji aweze kuwa na alama ya ubora katika bidhaa yake anatakiwa kumiliki
leseni ya alama ya ubora kutoka shirika la viwango Tanzania (TBS). hivyo basi, zipo
hatua mbalimbali ambazo mzalishaji hupaswa kuzingatia kabla ya kupata leseni ya
kutumia alama ya ubora ya TBS kwenye bidhaa yake.
Hatua ya kwanza ni maombi ya uthibitishaji ubora ambayo hufanywa na mwombaji
kwenda kwa Mkurugenzi Mkuu wa shirika la viwango Tanzania kwa maandishi. Majibu
hutolewa yakielezea taratibu za kufuata na gharama zote zinazohitajika.
Majibu hayo huambatana na fomu maalum ambayo mwombaji huijaza na kuirudisha
TBS ikiwa na viambatanisho vifuatavyo: mtiririko wa uzalishaji wa bidhaa husika, mfumo
wa uongozi ukionyesha kitengo cha udhibiti ubora, orodha ya malighafi anazotumia na
mahali zinakotoka kwa kila bidhaa pamoja na ramani inayoelekeza jinsi ya kufika
kiwandani kwake.
Baada ya kutekeleza na kuwasilisha nyaraka hizo, tarehe ya kufanya ukaguzi wa awali
hupangwa. Izingatiwe kuwa mwenye kiwanda anatakiwa kuwa katika uzalishaji siku ya
kufanya ukaguzi wa awali.
Hatua inayofuata ni ukaguzi wa awali, ambayo ufanywa na wakaguzi wa TBS. ambapo
sampuli uchukuliwa na kupimwa ili kuona kama bidhaa inakidhi matakwa ya kiwango
husika. Mkaguzi huandaa taarifa kuhusu hali halisi ya kiwanda na mambo yanayostahili
kurekebishwa.
Hatua ya tatu ni upimaji wa sampuli zilizochukuliwa, na upimaji huo unafanyika katika
maabara za shirika la viwango Tanzania kwa kufuata kiwango husika. Baada ya kazi ya
upimaji kumalizika, ripoti hutolewa kwa mwombaji.
Hatua ya nne na ya mwisho ni utoaji wa leseni: uamuzi kuhusiana na kutoa ama
kutotoa leseni ya kutumia alama ya ubora hutegemea tu ripoti ya ukaguzi wa awali wa
kiwanda pamoja na ripoti ya maabara.
Kimsingi ripoti zote mbili zinatakiwa kuonyesha kwamba mazingira ya uzalishaji
kiwandani, mfumo wa uzalishaji na bidhaa iliyopimwa havina matatizo. Ikiwa sivyo basi
mzalishaji hutakiwa kufanya marekebisho na baadaye mkaguzi wa TBS hutumwa tena
na kuleta sampuli nyingine.
Vilevile, serikali imejaribu kutenga fungu kila mwaka kwa ajili ya wajasiriamali wadogo
na wa kati na kati ya hao wajasiriamali hao wanaweza samehewa kulipa ada yoyote
wanapoomba bidhaa zao kuthibitishwa ubora.
Hivyo basi, mjasiliamari ili kuweza kupata msamaha huo anatakiwa kupata barua ya
utambulisho kutoka ofisi ya SIDO iliyokaribu au chama cha wazalishaji mfano TAFOPA.
Taarifa fupi kutoka idara ya Afya iliyo karibu na mahali pa uzalishaji au cheti cha TFDA
kwa wale wanajihusisha na uzalishaji wa chakula huhitajika.
Muda wa alama ya leseni hiyo hudumu kwa mwaka mmoja. Na baada ya kupata leseni
ya kutumia alama ya ubora wanapaswa kutunza taarifa za uzalishaji na mauzo ambazo
zitahitajika kwa ajili ya ukaguzi wa baadae ukataofanywa na shirika.
Ili uendelee kudumu sokoni na kufanikiwa sana kibiashara alama hii ya ubora ni kitu
muhimu sana kwako mzalishaji na mteja pia.
KWA MAWASILIANO|;
ADVOCATE JUSTINE KALEB
CEO/LEGAL CONSULTANT
MORIAH LAW CHAMBERS,
MAVUNO HOUSE - POSTA MPYA,
(OPPOSITE TO GAPCO PETROL STATION),
1ST FLOOR - OFFICE NO. 102,
P.O. BOX 70849,
DAR ES SALAAM - TANZANIA - EAST AFRICA.
MOB: +255 755 545 545 600 / +255 713 636 264
TEL: +255 222 110 684
FACEBOOK: Moriah Law Chambers
No comments:
Post a Comment