.

.

.

.

Thursday

Askofu Mokiwa kuhudhuria mazishi ya Jaji Lewis Makame

Askofu Mkuu mstaafu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Dk. Velentino Mokiwa, anatarajia kushiriki katika mazishi ya Mwenyekiti mstaafu wa tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Lewis Makame,aliyefariki dunia Jumatatu iliyopita.

Hayo yalisemwa na mtoto wa mrehemu, Morris Makame, jana nyumbani kwa marehemu maeneo ya Mbaramo wilayani Muheza, Tanga.

Alisema kuwa askofu huyo ni miyongoni mwa viongozi wakuu ambao watashiriki misa ya mazishi ya baba yake yanayotarajiwa kufanyika Jumamosi.

Morris alisema viongozi wengine wa dini  ambao watashiriki mazishi hayo ni pamoja na Askofu wa Anglikana Dayosisi ya Tanga, William Mahimbo Mndolwa na Askofu mstaafu wa Dayosisi hiyo, Philip Baji.

Alisema pia watakuwapo viongozi wa dini mbalimbali kutoka ngazi za juu  taifa na mkoa.

Morris alisema mwili wa marehemu baada ya kuwasili Muheza kutoka Dar es Salaam  utapelekwa nyumbani kwake maeneo ya Mbaramo  ambako itafanyika misa ndogo.

Alisema baada ya misa hiyo, msafara utaanza kuelekea kijijini kwao maeneo ya Tongwe wilayani na kufanyika misa kubwa ya mazishi katika Kanisa la Mtakatifu Yusuph. 

Mjukuu wa marehemu, Enersti Makame, alisema kuwa kwa sasa wanafanya maandalizi ya kujenga mahema nyumbani kwake Mbaramo mjini Muheza na kijijini Tongwe.

Alisema kuwa tayari wageni mbalimbali kutoka mikoani wameshaanza kuwasili wilayani Muheza wakiwamo ndugu na jamaa.

Enersti alisema magari zaidi ya 100 ya viongozi mbalimbali yataanza kuwasili kuanzia kesho wilayani Muheza kushiriki mazishi hayo.

SOURCE: NIPASHE

No comments:

Post a Comment